Kumekuwa
na malalamiko mengi kutoka kwa wafanyabiashara kuhusiana na wateja kudharau biashara
zao au hata kutopata wateja wanaothamini biashara zao. Hii inatokana na sababu
kadhaa ambazo huenda zikawa upande wa mfanyabishara au hata mteja mwenye pia.
Kuna mambo
kadhaa ambayomfanya biashara anatakiwa kuyafanya ili kuifanya biashara yake kuwa
na thamani kwa wateja au hata watu wengine.
1. Jina la Biashara.
Jina la
Biashara yako ndio kitu cha kwanza kitakachowafanya wateja na watu wengine
waithamini Biashara hiyo. Jina ni lazima liwe jepesi, fupi na lenye kuleta
maana nzuri kwa wateja uliowakusudia na jamii kwa ujumla wake. Ni lazima uwe na
jina la biashara litakaloendana na Biashara yako au kile unachokifanya kwenye
shughuli zako za kila siku au hata jina litakaloakisi sekta unayofanyia kazi.
Uchaguzi
mbovu wa jina unaweza kufanya watu wakaidharau biashara yako na wasiwe ni wenye
kuitilia umakini. Vilevile kufanya Biashara ambayo haina jina kunaweza
kusababisha ukose baadhi wa wateja ambao watahisi haupo serious na biashara
yako.
2. Machapisho.
Machapisho
yana umuhimu mkubwa sana kwenye kumfanya mtu aithamini biashara yako. Mbali na
kutumika kwenye kutangaza Biashara, pia machapicho yanaweza kutengeneza
picha nzuri kwa mteja na kumfanya ahisi kuwa upo makini na unachokifanya.
Machapisho
hayo yamejumuisha Vipeperushi, Business Cards, Mabango, Kalenda, Majarida,
Vitabu, Fulana, n.k. Vilevile unaweza kuchapisha nembo ya biashara yako sehemu
zingine kama vile kwenye kalamu, vikombe, au hata funguo.
Hii itafanya
watu waithamini biashara yako katika thamani ya hali ya juu.
3. Tovuti.
Tovuti hufahamika
kwa urahisi kama “Website”. Katika dunia ya leo mtu anaposikia au kuona
biashara yako na akavutiwa nayo, basi atakachofanya ni kuingia kwenye mtandao
na kutafuta tovuti yako ili ajue unachokifanya kwa undani.
Hivyo asipoona
tovuti yako kwenye mtandao hatoweza kufahamu unachokifanya na hii ndio itakuwa
hatua ya kwanza ya mtu kutoithamini biashara yako.
Vilevile
watu wengi inapowajia dhana ya kutaka kitu cha kununua huwa wanaanza kukitafuta
kitu hicho kwenye mitandao. Hivyo utakapokosa tovuti nzuri yenye utalaamu wa
kutosha, basi hakuna mtu atakayeweza kukufahamu na unaweza kukosa wateja wengi
sana kwenye biashara yako.
Ni vizuri
kwa mfanyabiashara kuwa na tovuti nzuri, yenye gharama nafuu, itakayoelezea
biashara yake kwa ujumla na hata kuweka baadhi ya ripoti na mafanikio
yanayohusiana na biashara yake hiyo.
4. Barua pepe.
Huenda kikaonekana
ni kitu kidogo sana, ila barua pepe (email) ni kitu cha muhimu sana kwenye
biashara za kileo.
Wafanya
biashara wengi katika zama zetu hupenda kutumia simu kwa kuwasiliana na wateja
wao. Ila ni lazima tutambue kuwa watu wengi hupenda kuulizia biashara kupitia
barua pepe na kueleza wanayoyahitaji pia. Hii hutengeneza mahusiano yako na
mteja ambapo mkishajuana vizuri ndio hufuata mazungumzo ya njia ya simu.
Hivyo ni
lazima kwa mjasiriamali wa kileo kuwa na barua pepe atakayotumia kuwasiliana na
wateja wake.
Hakikisha
unakuwa na barua pepe iliyokaa kiofisi zaidi. Usipende kutumia barua pepe zenye
@gmail.com, @yahoo.com, @hotmail.com. Barua pepe za namna hii huwa hazileti
mashiko na kwa wateja makini huenda ndio ikawa hatua ya kwanza ya kutothamini
biashara yako. Tumia barua pepe zenye jina lako la biashara hasa ile
itakayoendana na tovuti yako. Mfano marwa@tigo.com
No comments:
Post a Comment