Wednesday 20 April 2016

JINSI YA KUJIAJIRI BILA YA KUWA NA MTAJI WA PESA.


Assalaam Alaykum.

Vijana wengi wamekuwa na Hamu ya kutaka kujiajiri ili waweze kujiingizia kipato kitakachoweza kuwasaidia kujikimu katika maisha yao. Ila ukosefu wa Mitaji umeonekana ni kikwako kikubwa sana katika harakati hizo za kujiajiri.

Vifuatavyo ni vitu ambavyo mtu ambaye hana mtaji anaweza akafanya na akawa amejiari na kuweza pia kujipatia kipato Insha Allah.

1.       Ufundi Stadi
Ufundi stadi ni ufundi ambao mtu anaweza kutengeneza kitu chenye kuvutia na akauza kwa watu wengine watakaokipenda kitu hicho. Vipo vitu vingi ambayo mtu anaweza kutengeneza kwa mikono yake na akapata kipato kidogo kinachoweza kumfanya ajikimu na kikingine kuweka kama mtaji wa kukuzia bishara yake (Think Big). 
Mtu anaweza kutengeneza Fagio za Chelewa na kuuza mtaani. Pia vitu kama Makochi (Sofa Ste), Mazulia ya kufutia Miguu, Dawa za Asili ni vitu ambavyo mtu anaweza kujifnza kutengeneza na akaanza kuuza na kujipatia kipato cha kujikimu jata kama hana mtaji.

2.       Uza Vitu (au Huduma) kutoka kwa mtu Mwingine.
Hii ni njia nyingine ambayo mtu anaweza kujiajiri bila hata ya kuwa na mtaji. Wapo watu (au wafanyabiashara) ambao wanatafuta watu wa kuwauzia bidhaa zao kwa makubaliano ya kulipwa asilimia ya mapato (Commission) au hata kwa kumuacha mtu auze bidhaa kwa bei anayotaka na kurudisha kiasi atakachoambiwa arudishe kwa mwenye bidhaa. 
Hapa mtu ahitaji mtaji wa aina yoyote zaidi ya nguvu zake na muda wake wa kuuza bidhaa 9au huduma) husika.

3.       Uza Maarifa.
Hakuna mwanadamu ambaye hana maarifa (isipokuwa wale wenye matatizo ya akili). Mtu anaweza kuangalia maarifa aliyonayo kisha akayafanya kama mtaji na kuwauzia wengine. Mtu anaweza kuanzisha mafunzo ya masomo ya ziada kwa wanafunzi wa shule za msingi au sekondari na akaweka gharama ndogo za masomo hayo na akapata kipato.

4.       Badilishana na mtu kile ulichonacho.
Wengi wetu tunamiliki vitu kadhaa ambavyo vinathamani ambapo vikibadilishwa na vitu vingine vinaweza kutupatia kiasi kidogo cha pesa kinachoweza kutumika kama mtaji. Mfano wa vitu hivyo ni kama vile Simu za Mkononi, Laptops, n.k. Mtu anaweza kubadilishana vitu hivi na Pesa (aidha kwa kuuza au kuviweka Dhamana kwa muda) na akapata mtaji wa kuanzisha ajira yake binafsi.

Hizo ni baadhi tu ya njia zinazoweza kutumika kama ajira binafsi na kuweza kujiingizia kipato Insha Allah. Anza kuzitumia leo huku ukimuomba Mwenyezi Mungu akuongoze na kukusimamia uzuri katika kuzitumia njia hizo.

Maassalaam

No comments:

Post a Comment