Al-Huda Center of Islamic Banking & Economics (CIBE) ni taasisi inayojihusisha na utoaji elimu
na mafunzo juu ya masuala ya Kibenki na Kifedha kwa utaratibu wa kiislamu
duniani kote.
Kuelekea katika
harakati za kutimiza malengo yake, taasisi hii imeandaa mkutano mkubwa
unaokwenda kwa jina la "3rd African Islamic Finance Summit "
utakaofanyika siku ya Alhamisi na Ijumaa, May 19 & 20, 2016 katika hoteli
ya Hyatt Regency Hotel Dar Es Salaam.
Dhumuni
kubwa a mkutano huu ni kuelezea fursa mbalimbali zinazopatikana barani Africa
na kujadili changamoto zinazokwamisha ukuaji wa masuala ya kibenki na mifumo ya
kifedha ya kiislamu barani Africa.
Kwa
maelezo zaidi kuhusu usajili na taarifa za undani juu ya mkutano huu bonyeza
hapa.
No comments:
Post a Comment