Monday 16 May 2016

MKUTANO MKUBWA WA KIMATAIFA KUHUSU MIFUMO YA KIFEDHA YA KIISLAMU



Al-Huda Center of Islamic Banking & Economics (CIBE) ni taasisi inayojihusisha na utoaji elimu na mafunzo juu ya masuala ya Kibenki na Kifedha kwa utaratibu wa kiislamu duniani kote.

Kuelekea katika harakati za kutimiza malengo yake, taasisi hii imeandaa mkutano mkubwa unaokwenda kwa jina la "3rd African Islamic Finance Summit " utakaofanyika siku ya Alhamisi na Ijumaa, May 19 & 20, 2016 katika hoteli ya Hyatt Regency Hotel Dar Es Salaam.

Dhumuni kubwa a mkutano huu ni kuelezea fursa mbalimbali zinazopatikana barani Africa na kujadili changamoto zinazokwamisha ukuaji wa masuala ya kibenki na mifumo ya kifedha ya kiislamu barani Africa.

Kwa maelezo zaidi kuhusu usajili na taarifa za undani juu ya mkutano huu bonyeza hapa.


No comments:

Post a Comment